Mtume Paulo alitumia “kuenenda” mara nyingi katika maandiko yake, kuelezea safari yetu na Kristo.
Waefeso 5:15-16 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.”
Kuwa mwanafunzi wa Yesu sio tukio la mara moja au kitu tunachofanya kwa wakati fulani tu. Ni ushirika wa kila siku na Yeye. Ni hatua kwa hatua, mguu mmoja ukiufuatia mwingine katika mwendo wetu na Yeye, unaotupatia kukua kiroho. Inaanza kwa hatua ya kwanza ya wokovu na inaendelea kila siku kwa sisi kutembea pamoja na Kristo.
© Pastor Christine Mlingi